WALIMU NA SAFARI ZAO EP 2: Kelvin Mkulia: KWANINI WALIMU WENGI WANABAKI KUWA WA KAWAIDA.
Автор: Anna Shoma
Загружено: 2026-01-15
Просмотров: 134
Описание:
Kila mwalimu ana hadithi yake; wakati uliomvutia, changamoto iliyomjenga, mwanafunzi na matukio yaliyomkumbusha kwa nini anadumu kuwa mwalimu.
Katika mazungumzo haya, tunaleta hadithi hizo halisi. Ungana nami kusikia walimu wakisimulia safari zao binafsi, uhalisia wa darasani, na mafanikio madogo na makubwa yanayowapa nguvu ya kuendelea.
Mtazamo wa Kelvin juu ya namna ya kumjenga mwanafunzi ili kufikia hatma yake unavuka mipaka ya darasani na mazoea ya kawaida. Ni mtazamo unaomwona mwanafunzi kama mtu mwenye nafasi kubwa ya kufanikiwa sana kimaisha. Kupitia elimu, nidhamu ya kufikiri, na uongozi wa makusudi, Kelvin anaamini kila mwanafunzi ana nafasi ya kufikia kile alichokusudiwa kuwa.
Mtazamo wa Kelvin juu ya namna ya kumjenga mwanafunzi ili kufikia hatma yake, unavuka mipaka ya darasani na mazoea ya kawaida.
Je unajifunza nini kutoka kwake? Anakukumbusha jambo gani linalofanana na maisha yako ya kuwa mwalimu?
Karibu kuniandikia barua pepe [email protected] ili tusimulie safari yako pia. Kila siku, walimu tunayo nafasi ya kuboresha maisha yetu, utumishi wetu na maisha ya tunaowahudumia. Usiache kujifunza.
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: