DKT. BASHIRU APIGA MARUFUKU VIWANDA KUVUA, KULANGUA SAMAKI KWA WAVUVI
Автор: Wizara ya Mifugo na Uvuvi
Загружено: 2025-12-29
Просмотров: 3008
Описание:
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa amepiga marufuku viwanda vya kuchakata samaki nchini kuingiza mitumbwi yao majini kwa ajili ya kuvua au kununua samaki kwa wavuvi waliopo ziwani ambapo amesema kuwa hatua hiyo inavuruga soko, kuwafilisi na kuwafukarisha wavuvi.
Balozi Dkt. Bashiru amesema hayo mara baada ya kutembelea na kukagua kiwanda cha kuchakata samaki cha Nile Perch kilichopo Muleba mkoani Kagera Desemba 29,2025 ambapo ameongeza kuwa kitendo hicho kimekuwa kikifanywa na viwanda vyote vya kuchakata samaki nchini hatua ambayo ameeleza kuwa inawachochea wavuvi hao kufanya uvuvi usiofuata sheria kutokana na kukosa ushindani wa haki na kuwa na mapato madogo.
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: