Hoja Tatu za Tundu Lissu kwa Majaji Kesi yake ya Uhaini
Автор: GREEN FM TV
Загружено: 2026-02-09
Просмотров: 994
Описание:
Mwanasheria Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Dkt. Rugemeleza Nshala akizungumza na Waandishi wa Habari kwenye viunga vya Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Dar es Salaam leo, Jumatatu Februari 09.2026 amebainisha hoja tatu (3) zilizowasilishwa na Mwenyekiti wa chama hicho Taifa Tundu Lissu mbele ya Mahakama leo
Dkt. Nshala, amesema katika wasilisho lake Mahakamani, Lissu amewaeleza Majaji kuhusu mapito anayopitia gerezani ikiwemo uhuru na faragha ya kuzungumza na Mawakili na washauri wake wa sheria, kuzuiliwa kwa wanachama na viongozi wa CHADEMA wanaokwenda kumuona gerezani, sambamba na kucheleweshwa kwa kesi yake katika usikilizwaji kwani amekaa gerezani kwa siku zaidi ya 300 hadi sasa lakini kesi yake imesikilizwa kwa siku zisizozidi 15 hadi sasa
Sambamba na hilo, Mahakama leo imesikiliza hoja za Jamhuri katika mapingamizi yaliyowasilishwa na Tundu Lissu Novemba 12.2026, na imepanga kutoa uamuzi wa mapingamizi hayo Februari 11.2026
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: