SERIKALI YA ZANZIBAR ITAENDELEA KUUNGA MKONO JITHADA ZA MADAKTARI, KUWAPATIA HUDUMA ZA AFYA WANANCHI
Автор: Zbc Zanzibar
Загружено: 2023-03-12
Просмотров: 439
Описание:
Makamu Wa Pili Wa Rais Wa Zanzibar Mhe Hemed Suleiman Abdulla Ameyasema hayo katika hafla ya kuwashukuru Madaktari Wazalendo kutoka Tanzania Bara na Zanzibar huko Hoteli ya ngalawa, Wilaya ya Magharibi “A” Unguja ambapo alichangia Shilingi milioni 10 kusaidia huduma za Afya katika Bonanza maalum la kuchangisha damu.
amesema katika kuimarisha upatikanaji wa huduma za afya Serikali imeamua kujenga Hospitali za Kisasa kila Wilaya, na kuahidi kuzipatia Vifaa na Watumishi wanaohitajika katika Hospitali hizo wakiwemo Madaktari na Wauguzi.
Waziri wa Afya zanzibar Mhe. Nassor Ahmed Mazurui amesema kupitia Bonanza hilo Wizara imejifunza mambo mbali mbali na kuahidi kushirikiana na Wadau ili kutoa huduma bora za afya kwa Wananchi.
Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja Mhe. Ayoub Mohammed Mahmoud amesema jumla ya Wananchi elfu Tisa Mia Moja na Tisiini na Tano wamepimwa Afya zao na kupatiwa Matibabu na Chupa 349 za Damu salama zimepatikana.
Madakatari hao wameishukuru Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kushirikiana na Wizara ya Afya kwa kuwapa Ushirikiano na kufanikisha lengo lao la kutoa huduma kwa Wananchi wa Mkoa huo.
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: