WATOTO WA MASHIMBA WAIOMBA SERIKALI IINGILIE MGOGORO WAO WA ARDHI
Автор: Mwananchi Digital
Загружено: 2026-02-22
Просмотров: 1887
Описание:
Dar es Salaam. Wakati Neema Mashimba, mtoto wa aliyekuwa Mkemia Mkuu wa Serikali, Ernest Mashimba akiiomba Serikali kuingilia kati eneo lao lililotwaliwa na mfanyabiashara, Ally Rubea kwa madai amepangishwa kwa miaka 99, mlalamikiwa mwenyewe amejibu akisema aliuziwa eneo husika.
Akielezea hali ilivyokuwa, Neema amesema baada ya Rubea kuingia kwenye eneo lao lililopo Ploti Na 9 Ursino Estate Msasani Wilaya ya Kinondoni, kama mpangaji alibomoa nyuma yao na kufanya maegesho ya magari.
Kufuatia madai hayo, Mwananchi ilimtafuta Rubea ambaye amesema ukweli kwenye jambo hilo unapotoshwa kwani aliuziwa eneo hilo na familia baada ya kutangazwa kupitia madalali.
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: