RAIS MWINYI APOKEA OMBI LA KUJENGA NYUMBA ZA MAENDELEO - GAMBA
Автор: ASAM Online TV
Загружено: 2026-01-12
Просмотров: 1049
Описание:
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema Zanzibar imepiga hatua kubwa katika sekta ya elimu kwa kuweka mazingira mazuri ya kujifunzia kupitia ujenzi wa skuli za kisasa zenye hadhi na viwango vinavyokubalika.
Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo tarehe 10 Disemba 2026, alipozifungua skuli mbili za ghorofa ambazo ni Skuli ya Ramadhan Haji Faki iliyopo Gamba, Mkoa wa Kaskazini Unguja, pamoja na Skuli ya Kifundi kwa Niaba iliyopo Pemba.
Amesema Serikali inatambua mchango wa wananchi wa Gamba waliopisha ujenzi wa skuli hiyo na kuahidi kuwa Serikali inajipanga kufanya tathmini ili kuwalipa fidia zao stahiki. Aidha, Rais Dkt. Mwinyi amesema Serikali imepokea ombi la wananchi la kujengewa nyumba za maendeleo katika eneo hilo na kuahidi kulifanyia kazi.
Akitoa taarifa ya kitaalamu ya ujenzi wa Skuli ya Gamba, Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali, Ndg. Khamis Abdalla Said, amesema skuli hiyo imegharimu shilingi bilioni 11.2 na imejengwa na Kampuni ya ZECON, ikiwa na uwezo wa kuchukua wanafunzi 800 kwa wakati mmoja.
Ameongeza kuwa Skuli ya Kifundi ya Pemba imegharimu shilingi bilioni 9.4 na imejengwa na Kampuni ya SALEM Construction.
Skuli hizo zimejengwa kwa ushirikiano baina ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Benki ya Maendeleo ya Afrika (BADEA), ikiwa ni sehemu ya juhudi za Serikali kuimarisha sekta ya elimu nchini.
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: