ycliper

Популярное

Музыка Кино и Анимация Автомобили Животные Спорт Путешествия Игры Юмор

Интересные видео

2025 Сериалы Трейлеры Новости Как сделать Видеоуроки Diy своими руками

Топ запросов

смотреть а4 schoolboy runaway турецкий сериал смотреть мультфильмы эдисон
Скачать

SERIKALI YATOA BILIONI 6.8 MIKOPO YA ASILIMIA 10 MKOANI TANGA

Автор: TANGA MKOA TV

Загружено: 2026-01-05

Просмотров: 142

Описание: Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, Prof. Riziki Shemdoe, amesema kuwa Mkoa wa Tanga umefanikiwa kutoa mikopo yenye thamani ya shilingi bilioni 6.8 kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu katika kipindi cha mwaka wa fedha 2024/2025, tangu ruhusa ilipotolewa kwa Halmashauri kuanza kutoa mikopo ya asilimia 10.

Akizungumza wakati wa hafla ya utoaji wa mikopo hiyo mkoani Tanga, Prof. Shemdoe amesema kati ya fedha hizo, shilingi bilioni 3.8 zimetokana na makusanyo ya asilimia 10 ya mapato ya ndani ya Halmashauri, huku shilingi bilioni 3.4 zikitokana na marejesho ya mikopo iliyotolewa awali, jambo linaloonesha umuhimu wa urejeshaji wa mikopo kwa wakati.

Amesisitiza kuwa mikopo hiyo inaposisitizwa irejeshwe, lengo lake ni kuwawezesha wanufaika waliopo na vikundi vipya kupata fursa ya kukopa, akieleza kuwa urejeshaji mzuri wa mikopo utawezesha serikali kuongeza kiwango cha fedha kitakachotolewa katika miaka ijayo.

Katika hafla hiyo, serikali imetoa mikopo yenye thamani ya shilingi bilioni 2.761 kupitia Halmashauri za Jiji la Tanga, Lushoto, Korogwe na Pangani, fedha ambazo zimevikutanisha vikundi 155 vya wanawake, 71 vya vijana na 19 vya watu wenye ulemavu, na kutengeneza jumla ya ajira 1,715.

Prof. Shemdoe amesema utoaji wa mikopo hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa ahadi za Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan ndani ya siku 100 za kuimarisha uchumi wa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu kupitia mikopo ya asilimia 10.

Ameelekeza Wakurugenzi wa Halmashauri na Maafisa Masuhuli kuhakikisha mikopo yote inayotolewa inarejeshwa kwa wakati, huku Maafisa Maendeleo ya Jamii wakitakiwa kuhakikisha mikopo hiyo inawafikia wananchi katika kila kata, kwa kuwasaidia wenye uhitaji kujaza fomu za mikopo bila vikwazo.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Tanga, amesema kuwa tangu kuteuliwa kwa Mheshimiwa Rais, mkoa huo umeanza kutekeleza ahadi zake kwa vitendo, ambapo ndani ya kipindi cha chini ya miezi sita tayari shilingi bilioni 2.6 zimetolewa, na ifikapo mwisho wa mwaka kiasi cha mikopo kinatarajiwa kufikia takribani shilingi bilioni 8.

Nao wanufaika wa mikopo hiyo kutoka vikundi mbalimbali wameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita, wakisema mikopo hiyo imewawezesha kuanzisha na kupanua shughuli za kiuchumi, kuongeza kipato na kutoa ajira kwa vijana wengi.

Не удается загрузить Youtube-плеер. Проверьте блокировку Youtube в вашей сети.
Повторяем попытку...
SERIKALI YATOA BILIONI 6.8 MIKOPO YA ASILIMIA 10 MKOANI TANGA

Поделиться в:

Доступные форматы для скачивания:

Скачать видео

  • Информация по загрузке:

Скачать аудио

Похожие видео

NDC -TZ YAPONGEZA UWEZO WA BANDARI YA TANGA

NDC -TZ YAPONGEZA UWEZO WA BANDARI YA TANGA

MAMBO USIYOYAJUA KUHUSU MKOA WA TANGA,TABIA ZA WANAWAKE, MWANAUME KUHEMEA, ASILI YA JINA, MAKABILA

MAMBO USIYOYAJUA KUHUSU MKOA WA TANGA,TABIA ZA WANAWAKE, MWANAUME KUHEMEA, ASILI YA JINA, MAKABILA

Для Чего РЕАЛЬНО Нужен был ГОРБ Boeing 747?

Для Чего РЕАЛЬНО Нужен был ГОРБ Boeing 747?

ФИЛЬМ ПЕРЕВЕРНУЛ ВЕСЬ МИР! ТИХИЕ ВОДЫ Мелодрамы, фильмы новинки

ФИЛЬМ ПЕРЕВЕРНУЛ ВЕСЬ МИР! ТИХИЕ ВОДЫ Мелодрамы, фильмы новинки

LIVE: WAZIRI MKUU AMBANA RC CHALAMILA, ULEGA ISHU KIVUKO KIGAMBONI, WANANCHI WAMVA WAZIRI kutoa KERO

LIVE: WAZIRI MKUU AMBANA RC CHALAMILA, ULEGA ISHU KIVUKO KIGAMBONI, WANANCHI WAMVA WAZIRI kutoa KERO

🔥 СВЕЖИЙ ФИЛЬМ ДОЛЖЕН УВИДЕТЬ КАЖДЫЙ! НОВИНКА!

🔥 СВЕЖИЙ ФИЛЬМ ДОЛЖЕН УВИДЕТЬ КАЖДЫЙ! НОВИНКА! "Ищу Девушку с Голубыми Глазами" ВСЕ СЕРИИ ПОДРЯД

Mikopo ya Vikundi

Mikopo ya Vikundi

SHUHUDIA MRADI WA ULGSP, UNAVYOZIDI KUIPENDEZESHA HALMASHAURI YA MJI WA KOROGWE

SHUHUDIA MRADI WA ULGSP, UNAVYOZIDI KUIPENDEZESHA HALMASHAURI YA MJI WA KOROGWE

Губодутая жена - Русская мелодрама 2026, которая околдовала чужого мужа HD

Губодутая жена - Русская мелодрама 2026, которая околдовала чужого мужа HD

Daraja la mto Pangani na barabara katika ujenzi. Tanga Tanzania

Daraja la mto Pangani na barabara katika ujenzi. Tanga Tanzania

RC TANGA AWAASA WANANCHI KUSHEREKEA SHEREHE ZA MWISHO WA MWAKA KWA AMANI NA UTULIVU

RC TANGA AWAASA WANANCHI KUSHEREKEA SHEREHE ZA MWISHO WA MWAKA KWA AMANI NA UTULIVU

#TBC: RC MANYARA AHAMAKI MAMA MJAMZITO KUNYANG’ANYWA VITU KISA MUMEWE KUIBA SIMU!

#TBC: RC MANYARA AHAMAKI MAMA MJAMZITO KUNYANG’ANYWA VITU KISA MUMEWE KUIBA SIMU!

TANGA YAANDIKA HISTORIA MPYA YA KIBIASHARA

TANGA YAANDIKA HISTORIA MPYA YA KIBIASHARA

RIPOTI ZA SEMA AFRICA MEDIA  -  MKOWA WA KUSINI UNGUJA WAPATIWA  VIWANJA VYA MICHEZO.

RIPOTI ZA SEMA AFRICA MEDIA - MKOWA WA KUSINI UNGUJA WAPATIWA VIWANJA VYA MICHEZO.

RC SENDIGA AAGIZA UKAGUZI WA TAASISI ZA KIFEDHA | SASA OLE WAKO USIFUNGUE OFISI | TUTAWANYOOSHA

RC SENDIGA AAGIZA UKAGUZI WA TAASISI ZA KIFEDHA | SASA OLE WAKO USIFUNGUE OFISI | TUTAWANYOOSHA

BARABARA YA TANGA -  PANGANI YAANZA KUWEKWA LAMI

BARABARA YA TANGA - PANGANI YAANZA KUWEKWA LAMI

"HAPA HAROGWI MTU, MNATAKA NISEME MUANZE KUTISHIA KUTUROGA," RC SENDIGA BILA UWOGA AWAKA MANYARA

БЕСПЛОДИЕ, МАССАЖНЫЙ САЛОН И ТЮРЬМА 😳 ИСТОРИЯ ОДНОГО БРАКА, ПОРАЗИВШАЯ ВСЕХ | Русские мелодрамы

БЕСПЛОДИЕ, МАССАЖНЫЙ САЛОН И ТЮРЬМА 😳 ИСТОРИЯ ОДНОГО БРАКА, ПОРАЗИВШАЯ ВСЕХ | Русские мелодрамы

MBUNGE VITI MAALUM MOROGORO AWASHIKA MKONO WAATHIRIKA WA MAFURIKO KILOSA

MBUNGE VITI MAALUM MOROGORO AWASHIKA MKONO WAATHIRIKA WA MAFURIKO KILOSA

UZINDUZI WA MRADI WA UBORESHAJI WA JIJI LA TANGA

UZINDUZI WA MRADI WA UBORESHAJI WA JIJI LA TANGA

© 2025 ycliper. Все права защищены.



  • Контакты
  • О нас
  • Политика конфиденциальности



Контакты для правообладателей: [email protected]