MSIPORE ARDHI ZA WANANCHI KWA KIGEZO CHA UWEKEZAJI-DKT. MWIGULU
Автор: KASACO MEDIA (K.T.S)
Загружено: 2026-02-20
Просмотров: 4
Описание:
WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amewataka watendaji wa Serikali wasipore ardhi za wananchi kwa kigezo cha uwekezaji kwani msimamo wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kuwa kinara katika maendeleo na uwekezaji
“Rais Dkt. Samia anasema watendaji Serikalini, kwenye maeneo ya mikoa, wilayani msipore ardhi za watu kwa kigezo cha uwekezaji au maendeleo. Kila mtu apewe haki yake, msitumie ubabe kupora maeneo ya watu; Naibu Waziri - TAMISEMI andikeni barua inayotoa maelekezo hayo,” amesema.
Amesema hayo leo (Alhamisi, Februari 19, 2026) wakati akizungumza na wakazi wa Mkuu, mara baada ya kuweka jiwe la msingi kwenye jengo la utawala la Halmshauri ya Wilaya ya Rombo, mkoani Kilimanjaro.
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: