Mafarisayo [lyric video] - ABC Kilalani Choir
Автор: ABC Kilalani Choir
Загружено: 2026-02-16
Просмотров: 67
Описание:
MAFARISAYO ni wimbo wa kiinjili unaogusa moyo na kufunua hatari ya kujihesabia haki binafsi huku tukiwahukumu wengine. Unakemea unafiki wa kidini na kutukumbusha maneno ya Yesu kuhusu Mafarisayo waliokuwa wakisafisha nje lakini ndani wamejaa unafiki.
Wimbo huu unatufundisha kuwa Kanisa si mahali pa wakamilifu — bali ni hospitali ya kiroho ambapo walioumia, waliokosea, na waliovunjika hupata uponyaji. Yesu ni Tabibu wa karibu, mwenye rehema za milele, anayetoa dawa ya neema kwa kila anayemjia kwa toba ya kweli.
Kupitia sauti za kwaya ya ABC Kilalani , ujumbe huu unalenga kuponya, kurejesha, na kukaribisha walioko kando au waliovunjika moyo. Huu ni mwaliko wa kuacha kujihesabia haki na kumruhusu Kristo atusafishe kutoka ndani kwenda nje.
🎶 Kanisa ni hospitali — njoo upate dawa ya rehema.
#Mafarisayo #RehemaZaYesu #KanisaNiHospitali #ABCChoir #GospelYaKiswahili #UkweliWaInjili #WorshipKenya #ABCKilalani
📌 English Translation Version
MAFARISAYO translated ‘PHARISEES’ is a powerful gospel song that confronts the danger of self-righteousness while judging others. It exposes religious hypocrisy and reminds us of Jesus’ warning about the Pharisees who appeared clean on the outside but were filled with hypocrisy within.
This song teaches that the Church is not a place for the perfect — it is a spiritual hospital where the wounded, the broken, and the struggling find healing. Jesus is the Great Physician, full of eternal mercy, offering the medicine of grace to all who come to Him in true repentance.
Through the voices of the ABC Kilalani Choir, this message seeks to heal, restore, and welcome those who feel distant or burdened. It is an invitation to stop justifying ourselves and allow Christ to cleanse us from the inside out.
🎶 The Church is a hospital — come and receive the healing of grace.
#Pharisees #GraceOfJesus #TheChurchIsAHospital #ABCChoir #SwahiliGospel #GospelTruth #WorshipMusic #ABCKilalani
Recorded, mixed and mastered at Hitscore studios Nairobi Kenya
LYRICS👇🏾👇🏾👇🏾
MAFARISAYO
Afadhali mimi kuliko wale walioko makanisani
Mimi ni bora kuliko wale walioko makanisani.
Waongo wamejaa kule
Walevi wamejaa kule
Wasinzi wamejaa Kule
Afadhali mimi
Kuliko wale walioko makanisani.
Mafarisayo walikuwa watu wa ajabu sana
walijiwekea haki wenyewe
Mafarisayo walikuwa watu wa ajabu sana
Walijihesabia haki wenyewe
Walisafisha vikombe nje, na ndani vimejaa unafiki.
Yesu aliwaambia, mnafungia watu ufalme wa mbingu
Ninyi wenyewe hamuingii hamuendi
Na wanao ingia hamuachi waingie ee
Toa toa kwanza boriti lililo ndani ya jicho lako
Ndio uone vibanzi vilivyomo kwa wenzako
Kanisa ni hospitali
Twapata dawa kule
Twaponywa sisi kule
Afadhali mimi
Na uko kando na umelemewa
Yesu ni tabibu tena wa karibu
Rehema za daima ni dawa yake njema
Moyo wangu umepata pa kupumzika
Sio kwa mwingine ila ni kwa Bwana
Yesu ni tabibu, tena wa karibu
Rehema za daima ni dawa yake njema
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: