MVUA YAHARIBU BARABARA ARUMERU, WANANCHI WADAI AHADI YA BARABARA
Автор: ITV Tanzania
Загружено: 2026-03-11
Просмотров: 222
Описание:
#HABARI:Mvua zinazoendelea kunyesha zimeharibu vibaya barabara inayotegemewa na wananchi zaidi ya 2,000 wa vijiji vya Kata ya Kikatiti wilayani Aumeru mkoani Arusha, ambao kwa sasa wanashindwa kuzifikia huduma za muhimu zikiwemo za afya, na wameiomba serikali kutimiza ahadi yake ya zaidi ya miaka mitano sasa ya kutengeneza barabara hiyo .
Wakizungumzia tatizo hilo baadhi ya wananchi hao, wameomba mamlaka zinazohusika kuchukua hatua za dharura, ili waendelee kuitumia barabara hiyo wakati wakisubiri utekelezaji wa ahadi wanazopewa kwani usafiri wa pikipiki wanaotumia sasa unahatarisha maisha yao.
Akizungumzia malalamiko hayo kwa njia ya simu, Meneja wa TARURA Mkoa wa Arusha Mhandisi Nicholas Francis, amekiri kuwepo kwa ahadi ya kutengeneza barabara hiyo na kwamba wanachosubiri ni upatikanaji wa fedha.
Powered by #MCHEZOSUPA
JINSI YA KUSHIRIKI MCHEZO SUPA:
-
📱Tuma 1000 kupitia Airtel Money, Tigo Pesa, M - Pesa, Halopesa, kwenda namba ya kampuni 222223 📱kumbukumbu namba ni 777 au weka neno ITV.
#ITVDigital #ITVUpdates #ITVTanzania
#Follow @itvtz @radioonetanzania
@capitaldigitaltanzania.
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: