WAFAHAMU KUKU WA KIENYEJI AINA YA MWENDOKASI (audio Documentary )
Автор: Kuku Village Farm
Загружено: 2023-04-26
Просмотров: 6186
Описание:
Jiunge Na Group letu la Mwendokasi
https://chat.whatsapp.com/C17Bh4k1SH7...
WAFAHAMU KUKU WA AINA YA MWENDOKASI WANAOZALISHWA NA KUKU VILLAGE*
MWENDOkasi ni kuku Aliyeboreshwa Mwenye asili ya Kienyeji wa Tanzania (ambao ni Kienyeji wa Kisukuma pamoja na Kienyeji wa Horas. Lakini akafanyiwa Uborashaji Zaidi ili kumuwezesha Kuwa na Uwezo wa Kutaga Sana na Awe Anakua Haraka, ili afae kwa nyama pia. Ni mbegu ambayo hukua haraka sana, hutaga mayai 250 na kuendelea kwa mwaka, ni kuku ambao wana nyama tamu zaidi ya Kienyeji wa kawaida, ni kuku ambao wanastahimili magonjwa na ni kuku ambao wanakuwa na Nyama nyingi na maumbo makubwa bila kusahau huweza kufikisha hadi kilo 5 ndani ya miezi 6 au 7.
Kuku wa MWENDOkasi ni kuku wanaopatikana kuku village pekee kwani wao ndiyo waliofanya utafiti wa mbegu hiyo na kupata aina , muonekano na sifa za kuku hao ambao kutokana na sifa zao za ukuaji na utagaji walipewa jina la MWENDOKASI
Lengo la kupata MWENDOkasi lilikuwa ni kuangali namna tunaweza ingia sokoni na kuku bora anayekua haraka, Mrefu , Mstahimilivu wa Magonjwa, Mtagaji sana, anayetaga Mayai Meupe, Medium Size na yaliyochongoka, na bado akipata hizo sifa zote asipoteze ladha, na muonekano wa wa Kuku wa Kienyeji .
Ndiyo maana tukapata MWENDOkasi.
Kiufupi tunaweza sema MWENDOkasi ni kienyeji wa kibiashara . Kwani malengo ya Kumzalisha ni kuchukua nafasi pana ya Kuku wa Kienyeji katika Utagaji zaidi na ukuaji zaidi bila Kuathiri Ubora Wa kuku wa Kienyeji.
Kingine MWENDOkasi anafugika katika mazingira yoyote, iwe ndani, huria na nusu huria. Pia ukimfugia nje akapata Majani ya kutosha huwa anakuwa na Nyama na Mayai ya njano.
Bila shaka utakubaliana na mimi kuwa katika soko la kuku, kuku wa kienyeji ni dhahabu, hasa mijini. Kwani ana bei kubwa na hapatikani kwa wingi. Sasa wewe utakayefuga MWENDOkasi hii itakuwa ni faida kwako kwani utazalisha kuku wengi sana, na utawauza kwa bei ile ile ya juu. Hivyo kufanikiwa zaidi kibiashara .
Pia kuna kitu ambacho wafugaji ni lazima wajue. Katika ufugaji ili upate matokeo bora ni lazima ufuge kitaalamu. Yani Chakula Bora, Chanjo, Usafi na biosecurity . Hivi vitu vitakusaidia ufike vizuri katika malengo yako. Jambo la msingi unalotakiwa kufahamu... ukifuga MWENDOkasi mpaka anafikisha miezi 4 au 5. Gharama zitakuwa around 3000* Mpaka 7000 * (gharama zitategemea na eneo ulilopo)
kwa kuku na ukimuuza ni kuanzia 10,000 Mpaka 25,000 inategemea na mahali ulipo. Pia mayai yake utauza 10,000 mpaka 18,000 Kwa Trei.
Kuku wetu wa MWENDOkasi, wanafikia umri wa kuliwa au kuuzwa kwa nyama wakiwa na miezi 2.5 mpaka 3, huku wakiwa na uzito wa 1.8kg kwa tetea na 2.3 kwa jogoo.
Kwa upande wa mayai kuku wa MWENDOkasi huanza kutaga wakiwa na wiki 18 yaani miezi 4.5. Na wakifikia peak ya utagaji huwez kutaga kwa asilimia 82 mpaka 88. Viwango ambavyo ni vya COMMERCIAL LAYERS
Kwenye Suala la kulalia kuku wetu wamegawanyika katika makundi mawili wapo wanaolalia na wasiolalia.. kwasababu Lengo la kupata MWENDOkasi ni sababu za biashara ya Mayai basi kuku wanaolalia huwa ni wachache. Na hii lengo lake ni kuwasaidia wanaohitaji Vifaranga na hawana mashine basi watatumia hao tetea katika kuatamia na kupata Vifaranga. Ila kama mteja atahitaji kuku wengi zaidi walalie basi kuku wetu huwa wanatabia ya kuambukizana tabia ya kulalia. Akiwaacha hao wanaolalia kwa muda mfupi atajikuta kuku karibia wote wameingia joto na kulalia. Ila kwa wale wateja wasiohitaji kulali . Huwa kuna namna ambayo huwa tunawashauri wafanye ili kuondoa hiyo hali na kumuepushia mteja hasara ya kulalia na kukata utagaji.
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: