Mhe Masoud, amesema Serikali itaendelea kuthamini mchango unaotolewa na vijana wa kujenga Taifa
Автор: OFISI YA RAIS TAMISEMIM ZANZIBAR
Загружено: 2023-01-02
Просмотров: 3766
Описание:
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ Mhe Masoud Ali Mohammed, amesema Serikali itaendelea kuthamini mchango unaotolewa na vijana wa kujenga Taifa katika ujenzi wa miradi ya Maendeleo hapa nchini. Akifunga mafunzo ya mkupuo wa 067 na 068 katika kambi ya JKU KAMÀ, amesèma ushiriki wa vijana hao katika kazi za kijamii na kitaifa, kumetokana na mafunzo ya uzalendo, ujasiriamali na stadi za maisha waliyopatiwa kwa kipindi cha miaka miliwi. Mhe Masoud amewataka vijana hao kuyatumia vyema mafunzo hayo katika maisha yao ndani ya jamii na kuhakikisha kuwa wanazingatia maadili ili jamii iweze kuishi katika hali ya amani. Katika risala ya wahitimu iliyosimwa na Abdillah Nassor Abdala, imeeleza kuwa wamepata mafanikio ya kujifunza kazi mbali mbali za uzalishaji, ujenzi na ufundi na kuziomba kampuni kutumia utaalamu walionao vijana hao. Nae Mkuu wa Jeshi la kujenga uchumi, Kanal makame Abdalla Daima, amesema jeshi hilo limekuwa na hazina kubwa ya kuwajengea uwezo vijana wa kuweza kujiajiri na kuajiri wengine.
Jumla ya vijana 400 wamekamilisha mafunzo yao yaliyoanza Januari 2022 hadi Disemba 31 2022.
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: